Miongoni mwa kampuni/majina ya bidhaa yanayobeba jina la Huawei na ZTE yanaonekana kufanya vyema katika soko la ushindani lakini mambo yamekuwa ndivyo sivyo na mamlaka husika imezipiga marufuku kampuni hizo nchini humo.
Mawasiliano ya aina yoyote ile ni muhimu na yamekuwa ni kitu muhimu tangu enzi na enzi, Huawei/ZTE hawafahamiki tuu kwa biashara ya simu bali pia wamekuwatoa huduma ya intaneti yenye kasi ya 5G huko Australia.
Mamlaka husika imeamua kuzipiga marufuku ZTE na Huawei kutoa huduma ya intaneti (5G) kwa kile ilichokiita ni kwa sababu za kiusalama. Huawei wamekuwa wakitoa huduma ya 5G upande wa intaneti kwa kampuni za simu huko Australia.
Mamlaka husika imeona ni bora izuie kampuni hizo kutoa husuma hiyo kutokana na kwamba kwa mujibu wa sheria za Uchina kampuni yoyote itapaswa kutoa ushirikiano kwa serikali pale itakapotakiwa kufanya hivyo.
Kwa mantiki hiyo ndio maana mamlaka ya Australia ikaona ni busara kuacha kufanya kazi na kampuni hizo kwa sababu inawezeka kufikia kipindi kampuni za mitandao ya simu ikashindwa kujilinda/kuzuia mwingiliano pale Huawei/ZTE zitakapotakiwa kutoa ushirikiano kwa Uchina.
Vyanzo: Engadget, Reuters