Moja ya siri kuhusu kufanikiwa kwenye biashara yoyote ile ni kuwa mbunifu na Halotel Tanzania wamekuwa wakitoa huduma ambazo zinatokea kupendwa na wateja hiyo kuifanya kampuni husika kuendelea wateja wapya na wa zamani.
Sio mara moja, mbili, tatu tumeshaandika habari kuhusu kampuni inayojishulisha na mawasiliano ya simu wenye ardhi ya Tanzania ambapo tangu kuanzishwa kwake imekuwa ikikuwa mwaka hadi mwaka. Utakumbuka karibu miezi miwili iliyopita Halotel Tanzania walizindua vifurushi vya “Royal” na “Tomato” ilivyolenga kuvutia na kufanya mawasiliano kuwa nafuu zaidi. Kufahamu kwa undani kuhusu vifurushi vya Tomato/Royal BOFYA HAPA.
Sasa mwezi Aprili 2019 kampuni hiyo ya mawasiliano nchini Tanzania wameboresha kifurushi cha Tomato kwa kumpa uwanja wa kuongea na mtu kwa njia ya simu bila kukuathiri sekunde izonunua kwa kila dakika tano za mwanzo kwa simu kutoka Halotel kwenda mitandao yote Tanzania.
Kifurushi hicho ambacho kimeboreshwa kinaitwa “TOMATO PLUS”. Baada ya kununua kifurushi hicho mteja ataweza kuongea BURE dakika tano (5) za kwaza bila kujali mtandao husika ambapo haijalishi namba ni ya Vodacom Tanzania, TTCL, Zantel, n.k.