Kampuni ya Halotel imetangaza kuondoa gharama za kutuma fedha huku ikiwazawadia muda wa maongezi wateja watakaoweka fedha kwenye akaunti zao.
Halotel inayokuwa kwa kasi imezindua kampeni mpya inayofahamika kama ‘Ninogeshe na Halopesa’ inayowapa pia fursa wateja wa kampuni hiyo kutuma pesa bure ndani ya mtandao (Halotel-Halotel) muda wowote.
Lengo ni kuhakikisha wateja wanakuwa na wigo mpana wa kufurahia na kunufaika zaidi na huduma za mtandao huo bila kuwa na wasiwasi wa makato kila wanapotuma fedha mahali popote, wakati wowote.
Licha ya kuondoa gharama za kutuma fedha kutoka Halopesa kwenda Halopesa, pia wateja watapata muda wa maongezi wa bure kila wanapoweka fedha kwenye akaunti zao:
Mteja atakapoweka kuanzia Tsh. 1,000 kwenye akaunti yake kupitia wakala wa HaloPesa atazawadiwa muda wa maongezi huku akiendelea kunufaika kwa namna mbalimbali kila anapotumia huduma hiyo.