Uwepo wa njia mbalimbali za kuweza kutafuta kitu mtandaoni unampa mtu uwanja mpana wa kuchagua njia ya kutumia kutafuta kile anachokikusudia mtandaoni.
Kufanya mambo mseto inapendeza hasa ukizingatia na ukubwa wa kitu au jambo ambalo linasababisha kufikiria kuchangamana. Microsoft ni moja ya kampuni kubwa duniani na SwiftKey ni bidhaa iliyo chini ya Microsoft ikiwa kama programu tumishi ambayo ni mahususi kwa ajili ya kuweka nakshi nakshi kwenye kicharazio cha mguso. Lakini pia kama ni kutafuta kitu kwenye mtandao sio kitu cha ajabu kabisa ukijikuta ukiperuzi cha Bing.
Haifahamiki kwa wengi sana kuhusu mpango wa kimya kimya kuongeza “Google” kama kisaidizi cha kutafuta kitu kwenye mtandao na hivyo kutoa uwanja mpana wa mtu kuchagua kutumia Bing au Google.
Uzuri wa SwiftKey ni kuwa na uwezo wa kuongeza/kupunugza upana kicharazio kwenye programu husika lakini vilevile imeepushaa mtu anayeperuzi kutohamahama akijaruibu kuperuzi. Vipi wewe ni kati ya wale ambao wanatumia SwiftKey?
Vyanzo: Neowin, Android Police