Kwa miaka kadhaa sasa Google wamekuwa wakitoa bidhaa ambazo zinalenga kusaidia/kurahisisha upatikanaji wa vitu mbalimbali bila shida yoyote kwa mtoto aliye masomoni.
Kama ni mfuatiliaji mzuri wa masuala ya teknolojia utakuwa unafahamu kuhusu “Google Classroom” ambayo kwa sasa imeboreshwa ikiwapa nguvu zaidi walimu kuhakikisha mwanafunzi anatumia akili yake mwenyewe kuweza kufanya vizuri katika masono yake.
Google Classroom ni nini?
Google Classroom ilianzishwa mwezi Agosti, 12 2014 ambapo ni programu tumishi/tovuti (darasa) unaomuwezesha mwalimu kuwasiliana na wanafunzi wake/kuweka mazoezi, maandiko ya kujisomea na hata kuweka alama alizopata mwanfunzi.
Sasa katika masasisho mapya yaliwekwa kwenye programu hiyo imewaongezea uwezo walimu/wazazi kuweza kuzima programu tumishi/vivinjari wakati ambao mwanafunzi anapaswa awe amelala au anapotakiwa kuelekeza akili kwenye masomo yake.
Vilevile, mwalimu pia ana uwezo wa kuzuia mwanafunzi asiweze kutumia intaneti kuweza kutafuta majibu ya maswali wakati ambapo anafanya mazoezi jambo ambalo linamfanya mwanafunzi atumie akili yake tu kuweza kufanikiwa (kupata majibu ya maswali aliyoulizwa).
Kutokana na ukuaji wa teknolojia pamoja na utandawazi imekuwa ni changamoto kuweza kufanikisha mwanafunzi asiweze kuibia lakini kwa hiki ambacho Google wamekiboresha inavutia.
Kama mtoto wako anatumia Google Classroom hakikisha haachi bali anaendelee kuitumia kila siku kwani itamsaidia. Wewe je, una mawazo gani?
Vyanzo: The Verge, Gadgets 360
One Comment
Comments are closed.