Katika moja ya vitu ambavyo Google wanastahili pongezi baada ya kufuata nyayo za wapinzani wao wakubwa kwenye biashara ya masuala ya teknolojia ni kuwa na kisaidizi binafsi cha kwao wenyewe (Google Assistant) kama ilivyo kwa Apple na SIRI.
Ni hivi leo tu Google imewezesha ‘msaidizi binafsi kutoka Google’ maarufu kama Google Assistant kuweza kujua ni wimbo gani unaimba kwa wakati huo kwenye simu yako kwa maana ya kwamba jina la wimbo husika pamoja na jina la aliyeuimba na mengineyo mengi tu.
Kwa kusema “What song is this?” Google Assistant itaweza kukwambia jina la wimbo, msanii aliyeimba wimbo husika, jina la albamu pamoja na link mbalimbali kuhusiana na wimbo huo mathalani kwenye Youtube.
Hapo awali wenye simu mpya kutoka Google ndio pekee ambao masasisho hayo waliyakuta kwenye simu hizo mpya kutoka Google lakini hivi sasa ni kwa yeyote yule anayetumia Google Assistant. Kwa wenye simu za Google Pixel 2s nchini Marekani wakiuliza jina la wimbo husika, Google assistant inalinganisha mdundo wa wimbo husika na zaidi ya midundo laki moja iliyonayo kwenye kumbukumbu zake bila uhitaji wa intaneti.
Kwa wenye simu za Google Pixel 2s nje ya Marekani watahitaji kutumia intaneti ili kuweza kupata majibu ya wimbo waliomba kupatiwa majibu kwenye kwa kutumia Google Assistant.
App ya Shazam imeonekana kupata mpinzani kwani hivi sasa nayo Google Assistant pia inaweza kufanya kile ambacho kilifanya watu wapakue app ya Shazam kwenye simu janja zao. Je, kwa hili sasa litakufanya uwe karibu zaidi na Google Assistant?
Vyanzo: The verge, Engadget
2 Comments
Comments are closed.