Mradi wa kuunda gari lenye kasi zaidi duniani umefufuliwa na tayari gari hilo limeshavunja rekodi ya kwenda maili moja ndani ya sekunde 3.6 🙄 🙄 🙄 .
Mpango wa kuunda gari hilo lililopewa jina ‘Bloodhound’ ulikwama miezi ya karibuni kutokana na matatizo ya kifedha lakini mfadhili mpya amepatikana na tayari limeshaweka rekodi likiangazia kuweka rekodi nyingine mwaka huu.
Mwezi Oktoba 2017 ni historia ya miaka 20 tangu kuwekwa kwa rekodi ya sasa ya kasi ya gari ardhini ambayo ni Kilomita 1,228 kwa saa (763mph). Rekodi hiyo iliwekwa na gari lililopewa jina “Thrust SSC” jangwani Nevada-Marekani.
Katika maajribio yatakayofanyika majira ya joto mwaka huu wa 2018 linaangazia kwenda umbali wa 1000mph.
Gari hilo linaundiwa Uingereza na liliwasilishwa kwenye maonyesho Canary Wharf, London likiwa bado halijakamilika mwezi Septemba mwaka jana na tangu wakati huo limekuwa Bristol likiwa halifanyiwi kazi yoyote.
Gari hilo litatumia injini ya ndege aina ya injini ya Rolls-Royce Ej200 jet fighter pamoja na roketi kadhaa zilizoiwezesha kwenda umbali wa maili moja ndani ya 3.6.