Imeelezwa kuwa WhatsApp sasa wana mpango wa kuongeza vipengele vipya zaidi viwili lengo ni kuzidi kuifanya programu tumishi hiyo kuwa bora zaidi kwa watumiaji wake.
Kipengele cha kwanza ni “Mark As Read” ambapo kitamuwezesha mtu kuweka kuruhusu meseji kuwa tayari amesoma bila kuifungua, ikitokea katika sehemu ya taarifa fupi (notification bar).
Kipengele cha pili ni “Mute” ambacho kitamuwesha mtu kuweza kuzima kupokea taarifa fupi bila kufungua WhatsApp; kwa ule ujumbe mfupi ambao unasomeka kikamilifu bila kufungua ndani hapa ndio mahala pake.
Baada ya kukosolewa vikali juu ya usambaaji wa taarifa za uongo kupitia WhatsApp, wameamua pia kuachia kipengele kipya ambacho kitatoa taarifa na kuonesha juu ya meseji ambazo imetumwa na mtu kama kaandika mwenyewe au kachukua kutoka sehemu nyingine (forwaded).
Sio kwa jumbe tu (messages) bali hata kwa picha na video, kipengele hicho kitafanya kazi ya kukuonesha uhalali na usahihi wa kitu kilichotumwa. Lakini pia, kwa upande wa usambazaji wa Links, itaweza kukujulisha kwa kukuwekea alama nyekundu kukuonesha kuwa makini na taarifa hiyo kabla hujaifungua.