Itamlazima mtu kuwa anayependa kuja vitu vinavyohusiana na teknolojia kwa ukaribu zaidi kuweza kujua neno “eSIM” lina maana gani na ufahamu wa watu kuhusiana na kitu hicho.
eSIM imekuja kuonekana kwenye simu mpya za iPhone kwa mwaka 2018 nikimaanisha iPhone XS na iPhone XS Max lakini teknolojia hiyo ipo kwenye nchi takribani kumi mpaka hivi sasa.
Je, eSIM ni nini hasa?
Neno eSIM kirefu chake embedded SIM kwa tafsiri rahisi lakini isiyo rasmi ni kadi ya simu iliyojengewa ndani ya simu (haiwezi kutoka). Hii ina maana ya kwamba haitawezekana kubadilisha kadi ya simu kutoka mtandao mmoja hadi mwingine.
Dalili za ujio wa teknolojia hiyo zilianza kuonekana kwa mara ya kwanza kwenye saa janja Apple Watch 3 jambo ambalo liliweza kuibuka na kuamini kuwa eSIM ilikuwa ipo karibu kutumiwa kwenye bidhaa nyingine za Apple.
Kutokuenea kwa teknolojia husika.
Mpaka hivi sasa ni Austria, Canada, Croatia, Jamhuri ya watu wa Czech, Ujerumani, Hungary, India, Uhispania, Uingereza na Marekani ndio teknolojia ya eSIM ipo na inatumika.
Uchina itapokea toleo maalum la iPhone XS na XS Max ambazo kimsingi zitakuwa zikiwa na uwezo wa kubeba kadi mbili za simu lakini ile ambayo imejengegewa ndani kwa ndani itabidi ndio iwe kadi kuu.
Kama utakuwa na mpango wa kununua iPhone XS au XS MAx basi ndio ujue kuwa itakuwa teknolojia ya eSIM. Swali la kujiuliza Tanzania au nchi za Afrika tutaziweza simu hizo?
Vyanzo: The Verge, 9TO5Mac.