Kampuni moja ya madawa imepata kibali cha kufanya majaribio ya chanjo ya Virusi vya Zika kwa binadamu, majaribio haya ni ya kwanza na yanalenga kuona jinsi ambavyo dawa hii inapokelewa na miili ya binadamu.
Kama majaribio haya yatafanikiwa basi yatakuwa mafanikio makubwa katika kuelekea kuzuia kabisa gonjwa hili ambalo ni tishio kwa dunia. Mpaka sasa ugonjwa huu umesambaa zaidi katika nchi za Amerika ya kusini na pia Amerika ya kati.
Jarida la PHILADELPHIA limeripoti kwamba chanjo hii itajaribiwa kwa wafanyakazi arobaini ambao hawana maambukizi ya ugonjwa huo ili kuangalia jinsi miili itakavyo jibu baada ya kupewa chanjo hiyo. Huu ni utaratibu wa kawaida kabla ya chanjo kutumika kwa wagonjwa hujaribiwa ili kuona kama inamazara gani kwa binadamu wa kawaida.
Matokeo ya majaribo haya ya watu arobaini yatatangazwa baadae mwaka huu na matokeo haya yatatoa mwelekeo wa kufanikiwa ama kushindwa kwa chanjo hiyo.
Chanjo hii inatengenezwa na kampuni ya Inovio Pharmaceuticals Inc ambayo inashirikiana na GeneOne Life Sciences Inc, mnamo mwezi wa Februari shirika la afya duniani lilitangaza ugonjwa huu kuwa ni janga la dunia.