BoomPlay ni jukwaa kubwa la mtandaoni ambalo linakusadia kupakua na kusikiliza miziki na kutazama video kutoka kwa wasanii wako pendwa.
Mchango wa BoomPlay bila shaka umeonekana na hii imipelekea kunyakua tunzo kama App bora kutoka Afrika. Tunzo hizi zinatolewa na Apps Africa, ambayo ni tovuti inayojihusisha na habari za kitekinolojia na utoaji wa ushauri wa kitaalamu unaoangazia ufahamu wa maswala ya simu, tekinolojia na ubunifu.
App ya Boomplay Music inakuwezesha kupata nyimbo zaidi ya milioni , video za kutosha na habari kede kede za burudani.
App inaongeza watumiaji wake kila siku kutokana na huduma bora wanayoitoa. Mpaka kufikia mwezi Oktoba mwaka huu tayari App ilikua na watumiaji milioni 15, wakati kwa mwaka 2016 mwishoni walikuwepo watumiaji milioni 6 tuu.
Unaweza ukashangaa kwa nini idadi ya watumiaji inaongezeka?
Jibu ni kwamba, urahisi wakuitumia, mwonekano mzuri na ubunifu, haswa kwa namna inavyorahisisha upatikanaji wa muziki kwa mamilioni ya waafrika, na kuchochea wanunuzi wa muziki kuongezeka, wakati ikisaidia kupunguza uharamia kupitia mikakati mizuri ya kibiashara, kuhakikisha hati miliki zinalindwa kwa jitihada zote na pia hizi ndio sababu zilizofanya App ya BoomPlay Kushinda tunzo hiyo.
BoomPlay ilishindanishwa na App nyingi, zikiwemo Carter – Afrika kusini, Asorbia – Ghana, Truecaller Africa and FeastFox – Afrika Kusini. Mwisho wa siku ilitoka kidedea na kuwabwaga mbali wawaniaji wengine na kuwa App ya kwanza ya kupakua na kusikiliza muziki kushinda tuzo hiyo.
Wakati wanakabidhiwa Tunzo hiyo huko Afrika kusini, Mkurugenzi mkuu Bw. Joe He alisema: “Kunyakua tuzo ya Best African App kunaonyesha kufanikiwa kwa jitihada zetu za kujenga mfumo bora na endelevu kwa wamiliki wa kazi za sanaa ya muziki, wakati huo huo tukihakikisha kazi za sanaa ya muziki zinawafikia watumiaji kwa urahisi zaidi. Kwa kipindi kifupi tu cha miaka miwili mafanikio tuliyoyapata ni ya kuvutia”.
Kampuni inaamini kwamba wamiliki wa kazi za sanaa ya muziki wanaweza kufaidika na mauzo ya kazi zao. Zaidi ya watumiaji milioni 2 kwa sasa wanatumia app kusikiliza muziki, kutazama video na kusoma habari kila siku.
BoomPlay Kwa Android ingia hapa kuipakua
BoomPlay Kwa iOS ni mpaka 2018
TeknoKona inatoa pongezi sana kwa App ya BoomPlay Kwa kunyakua tuzo hii ya ubunifu (AppsAfrica Innovation 2017) kwa bara la Afrika.