Mapema wiki hii Samsung ilisema wazi kuwa wahandisi wa kampuni hiyo wanajimini kuhusu usalama wa betri la Samsung Galaxy Note 9 iliyozinduliwa karibuni.
Betri iliyo kwenye Galaxy Note 9 ni salama zaidi kuliko zilizopita hivyo watumiaji hawana haja ya kuwa na wasiwasi juu ya betri tena na kuanzia mwaka jana Samsung imeweka timu mpya ya udhibiti wa ubora ambayo itawajibika katika kuhakikisha kuwa bidhaa za kampuni zinakabiliana na miongozo ya ubora wa bidhaa zake.
Pia imefanya mabadiliko katika sehemu nyingine za mzunguko wa uzalishaji ili kuhakikisha hakuna kurudia kwa yale yaliyotokea kwa Samsung Galaxy Note 7.
Betri linalotumika katika Samsung galaxy Note 9 ni la Li-Ion na lina 4000mAh, kuweza kukaa na chaji kwa muda wa saa 72 bila ya kuchajiwa kwa matumizi ya namna yoyote yale.