Kwa mujibu wa tovuti moja ya nchini Poland imeripoti kupata bei ya simu ya Samsung Galaxy Note 9 kutoka kwa mmoja wa mwajiriwa wa kampuni hiyo aliyehudhuria kikao cha ndani kuhusu maandalizi ya uzinduzi wa simu hiyo.
Kwa mujibu wa mfanyakazi huyo bei ya Samsung Galaxy Note 9 yenye ukubwa wa uhifadhi wa ndani wa ukubwa wa 128GB na RAM GB 6 itakuwa ni $1,158 takribani shilingi za Tanzania 2,640,000.
Samsung Note 9 inatarajiwa kuzinduliwa rasmi Agosti 9 mwaka huu ikiwa na prosesa mbili tofauti za aina ya Exynos 9810 na Snapdragon 845 kulingana na soko na inaelezwa itakuja na rangi tano tofauti tofauti. Hata hivyo, bado haipo wazi ni rangi gani hasa itakazokuja nazo.