Unapokuwa unahangaika huku na kule unaweza ukawashangaza watu wengi kutokana na kile ambacho unakifanya mpaka hatua a kukiuka masharti yaliyowekwa, basi ndivyo walivyofanya Apple.
Apple, kampuni yenye thamani kubwa zaidi kwenye soko la biashara imeenda mbali na kuamua kutofuata kile ambacho wao wenyewe walikiweka kwa lengo kwamba kifuatwe lakini imewabidi waende kando kidogo ili waweze kutafuta wateja kinamna.
Iwapo tunatumia iPhone au bidhaa nyingine kutoka Apple bila shaka utakuwa unafahamu huduma ya Apple Music ambayo inatoa huduma za kusikiliza muziki, kuangalia picha jongefu bila kupakua, pia kusikiliza redio mtandaoni, n.k.
Sasa Apple wamekiukaje mwongozo?
Wakati mwingine inapobidi na ili mambo yaweze kwenda sawa kuna vitu ambavyo inakuwa ni sharti kuvifuata/kutekeleza. Kwa mujimu wa mwongozo wa App Store kipo kipengele kinachozungumzia kutotumia mtindo wa kutuma taarifa fupi zinazohusu kutangaza/kutaduta wateja wa kitu fulani, hapo ndipo Apple walipokiuka.
Hiyo ndio Apple ambayo mara moja moja inapindisha masharti kwa lengo fulani hasa wakiwa wanatafuta wateja kwani walishawahi kupeleka taarifa fupi kwa wateja wao kuhusu onyesho la Carpool Karaoke mwaka 2018.
Vyanzo: The Verge, Gizimodo