Mabadiliko ya teknolojia kwenye vitu mbalimbali yamekuwa yakiwaacha watu midomo wazi kwa kushangaa jinsi mambo yalivyobadilika mathalani siku hizi kuna “Saa janja” ambao ina uwezo wa kuongezwa umeme unapopungua/kuisha kabisa, kutuma/kupokea ujumbe mfupi maandishi au hata kupokea simu lakini kubwa zaidi kuweza kuokoa maisha ya binadamu.
Waswahili husema “Kizuri kinagharama”. Ndio, saa janja inauzwa kwa bei ambayo inaweza ikashangaza wengi hasa kutokana na udogo wa kitu chenyewe lakini ukijaribu kutaka kuijua vilivyomo ndani yake utashukuru na hasa katika ulimwengu huu wa teknolojia. Iwapo umeshawahi kumiliki/unamiliki saa janja unafahamu mbali na vikorombwezo vyote ilivyonavyo lakini ni kitu muhimu katika kusaidia kuangalia afya zetu.
Mtu mmoja aliyekuwa ameketi huku akiangalia runinga na saa (Apple Watch) yake akiwa ameivaa alipata taarifa fupi kupitia saa hiyo kuwa mapigo yake ya moyo yalikuwa yanaenda mbio na ndipo alipotoa taarifa, watu wa huduma ya kwanza walipofika walimkuta tayari yupo hoi na mwisho wa yote kuweza kuokoa maisha yake.
Hospitali ndio sehemu ya kupata majibu ya uhakika na mara baada ya kufanyiwa vipimo ikagundulika ni kweli mwanaume huyo alikuwa na tatizo kitu ambacho kilisababisha mapigo yake ya moyo kuongezeka lakini ilikuwa ni kitu cha kushtusha kidgo kwani vyumba vyote vinne kwenye moyo wa mhusika vilikuwa vinafanya kazi vyema na ndipo alipogudulika ana tatizo ambalo kwa lugha ya kitaalamu na kigeni linaitwa “Supraventricular tachycardia“.
Hata kama saa janja ni ghali lakini tujifunge mkanda na kuweza kununua saa za namna hiyo ili kuongeza mlinzi wa karibu kabisa kwa afya zetu kwani isingekuwa taarifa fupi aliyoweza kuipata mgonjwa basi asiweza kupata hata nguvu za kuweza kutafuta msaada mapema.
Vyanzo: GSMArena, Telegraph