Katika wanawake watano waliotokea kwenye maisha ya chini sana na kupambana mpaka kuwa moja ya watu mashuhuri lakini pia tajiri duniani huwezi kuacha kutaja jina la Bi. Oprah Winfrey.
Bi. Oprah ambae kwwa miaka mingi tu alikuwa akiendesha kipindi chake mwenyewe, The Oprah Winfrey Show na kuacha kurusha kipindi hicho miaka kadhaa iliyopita sasa Apple wameamua kukaa chini na mwanamama huyo ili watengeneze vipindi.
Katika kila kitu ni muhimu kufanya ukiwa umejidhatiti kwani Apple anapata upinzani mkali kutoka kwa Netflix, Amazon ambao wote hao wanafanya huduma kuangalia vitu mtandaoni (online streaming).
Hatua ya Apple kufanya kazi na Bi. Oprah itawaongezea wapenzi na wateja wapya na hivyo kutanua wigo wa watazamaji kwenye masuala ya kuangalia vitu mtandaoni papo hapo. Utakumbuka Netflix walitangaza kuwa watakuwa wakifanya vipindi na rais mstaafu Obama pamoja na mkewe.
Bi. Winfrey ni mwanamama aliyewapa nguvu kwa maneno yake, msaada wa hapa na pale mabinti, wanawake, wake kwa waume na watu mbalimbali duniani na kuamini kuwa hakuna kinachoshindikana chini ya Jua.
Apple hawajaweka kiasi ambacho wamemlipa Bi. Oprah kuweza kufanya nao kazi kwa zaidi ya mwaka mmoja lakini inaaminika kuwa ni kiasi kikubwa sana.
Vyanzo: Apple Newsroom, The Verge
One Comment
Comments are closed.