Toleo la Android 11 laendelea kusogea kwenye simu janja nyingi tuu za Samsung (Galaxy A20s na nyinginezo) ambazo kampuni husika imeziweka kwenye mapngo wa kupokea masasisho hayo kama ilivyo kwa rununu nyinginezo ambazo wanazitengeneza.
Karibu na mwishoni mwa mwezi Juni Samsung Galaxy A Tab 8.0 ilipokea masasisho ya Android 11 na wiki chache baadae Tab A 10.1 nayo imewezeshwa kuweza kuhamia kwenye toleo hilo la programu endeshi na watumiaji wake kuweza kufurahia yale ambayo yanapatikana huko.
Samsung Galaxy A20s
Simu hii ambayo pia ilizinduliwa mwaka 2019 imekuwa miongoni mwa zile simu janja ambazo Samsung imezipelekea Android 11 na kufanya idadi ya simu janja zenye toleo hilo kuwa nyingi (idadi yake ni ngumu kufahamika kutokana na wingi wa bidhaa zenyewe π π π ).
Toleo hilo kwenye simu janja tajwa linakuja pamoja na aina tofauti tofauti ya kufanya muonekano wa mbele na hata ndani kuwa wa kuvutia (UI 3.1) halikadhalika na masasisho ya kuboresha usalama wa bidhaa hizo yaliyotoka mwezi Juni.
Daima ni kitu kizuri kwa simu janja kuwezeshwa kuhamia kwenye toleo jipya la programu endeshi lakini siku zote tukumbuke kuhakikisha kuwa simu inakuwa na chaji zaidi ya 50%, kifurushi cha intaneti ambacho kinazidi GB 1.4 bila kusahau uwepo wa nafasi kwenye memori angalau GB 1.5 na zaidi.
Vyanzo: Gadgets 360, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.